Orodha Ya Forbes Ya Wasanii Wa Hiphop Wenye Pesa Zaidi


Diddy anaongoza kwenye orodha hii ya wasanii watano wa hiphop wenye pesa zaidi duniani. Pesa hizi hutokana na muziki na kazi au biashara zingine wanazofanya kujiingizia kipato.
1] Puff daddy mmiliki wa Revolt Tv, Bad Boy Records na mavazi ya Sean John anaongoza kwa kuwa  na thamani ya dola milioni 700. Mwaka jana alikuwa na milioni 580 na wanasema kazi na biashara zake ndani ya miezi sita zimeongeza dola milioni 120 nakufikisha 700.
Ukiacha nilivyokutajia hapo juu Pdd pia anasimamia kinywaji kikali cha Ciroc.
22] Dr Dre Producer na rapper amechukua namba mbili kwa kuwa na thamani ya dola za Kimarekani milioni 550. Pesa zake zinatokana na studio ya Aftermath, Earphones na Headphones za Beats by Dre na mikataba kibao ya matangazo chini yake.
33] Sean Carter aka Jay Z  Amekalia nafasi hii kwa utajiri wake mwenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 520. Zimetoka kwenye muziki, ziara za muziki, Wasanii na record lebel ya Rock Nation. Pia pesa anazopata kutoka timu ya kikapu ya Brooklyn Nets, Mavazi ya Rocawear na Live Nation kila biashara hapo imempa dola milioni 150 million.
44] Birdman ndio C.E.O Wa Cash Money ambayo pia inamiliki Young Money. Anathamani ya ola milioni 160
55] 50 Cent anabiashara nyingi kama Maji, Energy Drinks, Headphones, Bidha za G Unit, Muziki na anacholipwa kwenye Filamu. Anathamani ya dola milioni 140.