
Mwanzoni jina la album lilikuwa “King Push” na sasa inaitwa “Daytona” vile vile cover ya album hiyo
Cover mpya ni picha ya bafu la hotel aliyokuwa anakaa mwanamuziki nguli wa R&B, Whitney Huston wakati amejikita kwenye madawa ya kulevya (Swipe Left ➡️ kuiangalia)
Imeripotiwa kuwa picha ilipigwa mwaka 2006 lakini iliachiwa baadae baada ya kifo cha muimbaji hiyo wa “I will always love you” Pusha T amesema ilikuwa idea ya Kanye kutumia picha hiyo.
Akiongea na Angie Martinez, Pusha amesema Kanye alitoa hadi mkwanja wake mwenyewe kulipia haki za kuitumia picha hiyo. Amelipia zaidiaya Million 193 Tsh ($85K)
Whitney Huston alifariki mwaka 2012, mwili wake ulikutwa bafuni kwenye hoteli ya ‘Beverly Hilton’ na chanzo cha kifo chake kilikuwa madhara ya ugonjwa wa moyo wa ‘atherosclerotic’ na matumizi ya cocaine